SIMBA YAICHAPA AZAM FC, KOSI LA FADLU SASA LIMENOGA

preview_player
Показать описание
Wekunfu wa Msimbazi, Simba SC wameendelea kuonyesha ubora wao msimu huu wa mashindano 2024/25 wakiwa chini ya kocha, Fadlu Davids kwa kuibuka na ushindi wa tatu mfululizo katika ligi bila ya kuruhusu bao baada ya kuichapa Azam mabao 2-0 kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.

Katika michezo mitano, mitatu ya ligi na miwili ya Kombe la Shirikisho Afrika, Simba imefunga jumla ya mabao 12, ikiwa ni wastani wa kufunga mabao 2.4 katika kila mchezo (kwa ligi tu ina wastani wa kufunga mabao matatu kwa kila mchezo) huku nyavu zao zikiguswa mara moja tu (kimataifa) na ilikuwa dhidi ya Al Ahly Tripol ambapo hata hivyo katika mchezo huo waliibuka na ushindi wa mabao 3-1.
Рекомендации по теме