Vinara wa muungano wa OKA wapuuzilia mbali madai kwamba wameshurutishwa kumuunga mkono Raila

preview_player
Показать описание
Vinara wa muungano wa One Kenya Alliance wamepuuzilia mbali madai kwamba wameshurutishwa kumuunga mkono kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga kwenye azimio lake la kuwania urais kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022 . Wakizungumza kaunti ya Mombasa , vinara hao wakiongozwa na Musalia Mudavadi wamesema hakuna mazungumzo yaliofanywa kuhusu kumuunga mkono mwaniaji mmoja wakati wa mkutano wao na rais Uhuru Kenyatta,na kwamba ni kosa kwa baadhi ya vyombo vya habari kudokeza kwamba wanashurutishwa kumuunga mkono mwaniaji mmoja.
Рекомендации по теме