Chama cha Nark-Kenya chajiunga na mrengo wa OKA

preview_player
Показать описание
Mrengo wa OKA sasa umekaribisha chama cha Nark-Kenya kinachoongozwa na Martha Karua baada ya kuondoka kwa Musalia Mudavadi ambaye ameungana na naibu rais, William Ruto. Karua alitia saini mkataba na vinara watatu wa mrengo wa OKA ambao ni Kalonzo Musyoka, Gideon Moi na Cyrus Jirongo. Viongozi hao wanne wanasema mkataba wa muungano wao utawasilishwa katika afisi ya msajili wa vyama vya kisiasa tarehe-28 mwezi huu.

with KBC Online;

#KBCchannel1 #Nark-K #OKA
Рекомендации по теме