AIC Chang'ombe Choir (CVC) - MOYO (Official Live Video)

preview_player
Показать описание
#MOYO, ni wimbo wa Tatu katika IBADA YA MOYO WA SHUKRANI iliyofanyika 10 NOV, 2023 katika kanisa la AICT Chang'ombe, Sokota Temeke Dar es salaam.
Ndani ya wimbo huu AIC Chang'ombe Choir tunamshukuru Mungu kwa baraka zake alizotukirimia kwa zaidi ya miaka 35 tangu kuanzishwa kwa kwaya yetu.
Tunaamini wimbo huu utaenda kufanyika Baraka katika maisha yako. MUNGU AKUBARIKI.

LYRICS

Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani moyo unatunza mengi

Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani moyo unavumilia

Moyo umebeba jeraha zangu
Eeh Moyo umebeba huzuni zangu

Moyo umebeba furaha yangu
Eeh Moyo umebeba ushindi wangu

Kuna muda kinywa kinatabasamu lakini Moyo unalia
Kuna muda macho yanafurahi lakini Moyo unalia

Nitaulinda moyo wangu kuliko yote niyalindayo , niyalindayo,
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima , Za uzima, za uzima

Nitaulinda moyo wangu kuliko yote niyalindayo niyalindayo,
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima , Za uzima, za uzima

Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani Moyo unatunza mengi

Kama machozi yangeweza kusimulia
namna gani Moyo unavumilia

Linda Moyo wako kuliko yote uyalindayo
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima

MUNGU BABA nifute machozi yangu mimi
Waujua Moyo wangu nigange jeraha zangu nibaki

MUNGU BABA nifute machozi yangu mimi
Waujua moyo wangu nigange jeraha zangu nibaki

Special Thanks
AICT CHANG'OMBE CHURCH
Mch. Dr Joseph Mayala Mitinje

CREDITS.
Song writer - Elisha Gerlad
Music Team - Benjamin Makolobela (MD,MAIN KEYS)
Elisha Gurlaty (AUX 1)
Elia Mahuna (AUX 3)
Onesmo Peter (AUX 2)
Emmanuel Yusuph (BASS)
Daniel (LEAD GUITAR)
Mayala Bubele (TRUMPET)
Charles Stenson (TROMBONE)
Meshack Wilson (TROMBONE)
Eliya Makaya (ALTO SAX)
Raphael Luhende (ALTO SAX)
Samson Mathew (DRUMS)

Video production - CVC Media
Audio Mixing & Mastering Engineer - Tamie Bimha
Sound System, Backline, Lights, Stage - Haddypro Campany Limited
Project Manager - Dr.Elidady Msangi Ejazz01 Music Pro
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Wimbo uliobeba uponyaji hakika mbarikiwe maana huu wimbo unaweza sikiliza siku nzima moyo ukawa na amani kubwa

beatricemalle
Автор

Hakika Kristo mwenyewe ahusike ktk kuiponya mioyo iliyozimia na kujeruhika ktk changamoto yoyote ya kimaisha🙏

LydiaKashimba
Автор

Mtunzi elisha gelard mungu akutunzee popote ulipo huu wimbo umetubariki wengi❤

netim_officialtz
Автор

MUNGU Ugangae Mioyo Yetu Tuko Tayari Kupokea Ibaada hii Tuhudumie Bwana Tugange Jeraha zetu Tubaki Salama🙏

elishgurlat
Автор

Mungu ugange moyo wangu katika maisha yangu

mwl.ombimahenge
Автор

This song wrecked my heart into pieces and mend the pieces back together like a shining armor.Nimepitia mengi kwenye maisha yangu, nilihisi kuchoka lakini bado moyo wangu ulivumilia kwa hali zote. Nimelia mno😭😭😭.Lakini leo nimejifunza nitaulinda moyo wangu kuliko vyote vilindavyo, maana ndipo zitokako chemchem za uzima wangu🙌🏿.Ee Mungu nisaidie🙏.

mohamedlegacy
Автор

Niseme hivi,
Ole kwa mtunzi na mwandishi wa wimbo huu,
Ole kwa mwalimu aliyefudisha wimbo huu
Ole kwa waimbaji wote walioimba wimbo huu.
Ole kila mtu aliyeusikia wimbo huu ukiimbwa popote
KAMA MOYO WAKE UTAKUWA MBOVU. MAANA MANENO YA WIMBO HUU NI MAZITO MNO!

ANDREA-kpu
Автор

Mungu nigange moyo wangu, mpaka nimelia Mungu wajua Mapito ninayo pitia. Mungu awabariki sana CVC

HurumaMfelo
Автор

2025 niko hapa kupata wimbo wa faraja❤❤

scholarsticaoscar
Автор

God heal my heart, my testimony lies in the situation whereby i am rejected by all that is around me, Sickness all in my Household, Having a Physically challenged children, Sick mother struggling with cancer, My dad who was struck with Blindness Last Year, My heart Bleeds, Was Suspended from Work 2023, All my siblings dropped out of school for depending on me and now i have none. My heart bleeds, but in all I still sing Hallelujah

Blessing_Hurdley
Автор

Tuliokuja kuiangalia hii nyimbo baada ya usiku wa Tunzo za gospel gonga like hapa

Abel-bm
Автор

Mbarikiwa sana watumishi wa Mungu kazi yenu ni njema

adamndamayape
Автор

Mungu ganga jereha zangu nibaki salama

marystephen
Автор

Kuna muda kinywa kina tabasam😄 lakini moyo unalia😭

PASTORRICHARDJEREMIAH
Автор

Nifute machozi yangu Yesu unigange jereha nibaki salama

judithgodifrey
Автор

Katika nyimbo zote chag'ombe huy niwimbo wa kwaza mwimbo una nisogeza karib na mungu naliia tuuuu mungu awabarik katk uwimbaji wenu amin

NaahGroly
Автор

😢😢😢😢❤❤ eeh Mungu naomba ugange jeraha zangu ili nibaki salama 🙌🙌

polyjoh
Автор

I have cried in my life ooh but i wont cry no more in 2025.

SILO
Автор

Mungu kanipa wimbo, 😢 Yesu nigange hakika....

joycemakiya
Автор

Mungu wa mbinguni azidi kuwabariki maana mnafanyika baraka kwa watu wengi sana.
Kazi njema kwa uongozi wa kanisa na uongozi wa kwaya pamoja na watu wote waliohusika

KelvinMushi-strd
visit shbcf.ru