TOZO ZATEKELEZA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO MWANZA/ WASANII WAUNGA MKONO SERIKALI AWAMU YA SITA

preview_player
Показать описание
Waigizaji na Wasanii mbalimbali mkoaniMwanza, wamesema wanaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya sita kwenye ukusanyaji wa tozo na wao wako tayari kulipa tozo hizo kwa kuwa wanaridhishwa na jinsi zinavyotumika kwenye utekelezaji wa shughuli za maendeleo mkoani humo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti walipotembelea miradi maendeleo iiliyopo Mwanza, ikiwemo mradi mkubwa wa Uzalishaji maji uliopo chini ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Mwanza (MWAWASA), na Mradi mkubwa wa Stendi ya Mabasi, Wasanii hao wameipongeza Serikali kwa Utekelezaji wa miradi hiyo kupitia tozo za wananchi.
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Huo ujenzi ulikuwepo kabla ya tozo, acheni kudanganya watu

charleswarega