Salama Na MwanaFA Ep 10 | KARAMA Part 1

preview_player
Показать описание
#YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast

Listen our Podcast on

Weekend mbili zilitopita rafiki yangu Mwinyi aka Mpwa aka Cousin aka Hamis alikua akiadhimisha siku ya kuzaliwa kwake na alikua amefiksha umri wa kustahili kusherehekea kwa kweli na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa maisha, mke wake kipenzi alinipigia simu siku nne kabla ya birthday ya mumewe na kutaka tujumuike nae kum suprise, pia akaniambia ana kazi sana ya kuweza kukamilisha hilo tukio maana jamaa (Mwana FA) kashasema yeye hana mango wa kutaka shughuli, angependa maisha yaendelee tu kama kawaida. Pengine alikua akitarajia dinner nyumbani na mkewe na wanawe basi. So kukawa na zoezi hapo la kuhakikisha jamaa hasomi mchongo na kwamba zoezi ni lazima lifanikiwe. Malika binti yeke kwa kwanza ndo alikua amiri jeshi mkuu wa kuhakikisha Baba anarudi nyumbani by saa mbili usiku ili ale na familia chakula cha usiku. Suala hili lilizidi kuwa tamu pale Malika alipofanikiwa kutimiza ombi lake kwa Baba na sisi wengine ikawa rahisi kuibuka nyumbani na kumaliza mchongo mzima. Ulikua usiku mzuri ambao umeandaliwa kwa mapenzi mengi, na kila kitu kilipangwa kwa uangalifu by saa nne unusu tunaimba kata keki tule 😃. Ila kitu unique kabisa kwenye sherehe hiyo ilikua ni vipande vya karatasi ambayo tuligaiwa, vilikua na namba na namba yako ikitajwa basi kuna swali ilikua unatakiwa kulijibu, ili kuonyesha ukaribu wetu, unataka kujua mimi nilipata swali gani? Ok, swali lilikua ni kama nakumbuka siku yangu ya kwanza kukutana na Mwana FA!

Hiyo story itaendelea siku nyengine ila kwa sasa nikuambie tu mahusiano yangu na yeye Mwinyi. Tumekua pamoja naweza sema baada ya kukutana hapa mini Dar es Salaam mwanzoni mwa miaka ya 2000, sote tukiwa wembamba na watoto tu, ila bila ya shaka kila mmoja akiwa na nia na madhumuni ya kufika hapa tulipo na zaidi panapo majaaliwa, kuna smile flani ivi ambalo mpaka leo halijawahi kubadilika ndo ID yake pamoja na mwanya flani unaokamilisha muonekano wake, style za misuko ya nywele tofauti pia ilikua ikimtenganisha yeye na wanamuziki wengine, ila kikubwa zaidi ambacho kinamfanya yeye awe kasimama mbali na wenzake ni jinsi anavyoandika, anavyowasilisha na anavyowakuna pia washabiki wake ambao kila siku zinavyozidi kwenda wamekua wakiongezeka, nadhani ni baada ya kampa sikio la moja kwa moja ambako kumewafanya wamsikilize kwa umakini zaidi.

Siku za hivi karibuni rafiki yangu aliibua mjadala kwenye mitandao ya kijamii zaidi Twitter baada ya kuamua kujiita yeye Shaaban Robert wa enzi zetu, kama ulikua hufahamu Shaaban Bin Robert alikua mi mshairi, muandishi wa vitabu na essay na pia inaaminika alikua moja kati ya wafikiri wazuri wa lugha ya Kiswahili kutoka Afrika ya Mashariki. Mwana FA ni mmoja kati wa washairi wazuri na mwenye style tamu pia ya kuwakilisha uandishi wake kwa miaka mingi sasa ya muziki huu wa kizazi kipya. Kama unadhani anastahili kujiweka ligi moja au hata nyumba moja na Shaaban Robert au pengine hana nafasi hiyo mimi sina cha kusema juu ya hilo, ila ninaloweza kusema ni kwamba rafiki yangu huyu ameonekana kukua mbele ya macho yangu kwa zaidi ya miaka kumi na tano sana, alianza kufanya kazi zake mapema tu kama solo artist na ngoma sake ya kwana tu ilikua HIT, Unaikumbuka INGEKUA VIPI? Kisha ikaja ECT, baadae kama Duo yeye na AY huku akiwa anaendelea kufanya solo projects na baada ya hapo ameendelea kusimama mwenyewe na kujiimarisha kila mara anapotupa nyimbo mpya, na kwa hilo basi niko hapa kwaajili ya kutoa heshima zangu kwake na kumtakia kila lenye kheri naye.

P.S

Mwana FA pia ni rafiki mzuri na Baba kipenzi kwa mabinti zake.

Enjoy.

Love,

Salama.

Follow:
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Subtitle 1:24
Hali yangu si hayati si mamati,
kati kwa kati si mzima wa kutembea
sana wala mgonjwa waa kulala

christopherlusiga
Автор

Mwana FA napenda unavyojua kuongea na media be blessed na keep it up
Ww kama Ronaldo unajua kucheza na kamera

gastordominic
Автор

I like how Salama asks her questions...she exactly knows what we the audiences would want to know next from the person being interviewed. Big up Sally.

Amani
Автор

Iko hiv kama salama ni moja ya wanawak wabunifu, wasiokata tamaa, ni mpambanaj pia kwa kuongeza ladh kweny vipnd kam mkasi na mpka hiki yah ston town lov u so much, may god be with u salama**mwana fa secret super star pia ni bidhaa adim iliomuhim kweny mafunzo ya maisha

husseinmussa
Автор

Duh, FA amepitia maisha magumu, acha tu apumzike kwa kula raha now

mwandegeplaza
Автор

Nilisoma comment kwenye intavyuu ya Gigi kuwa intavyuu ingine nzuri ni ya Mwana FA na sasa naitizama...nimejifunza kwel usione mtu anafurahi kuna siri kubwa nyuma yake.Big Up kwa kaka Binamu na dada Salama.😍

esterdanford
Автор

Jamaa namuelewa sana et anajua vingi ila ajionyeshi

christopherjames
Автор

Hii ndio maana kaitwa Philosopher kweli hekima na busara ndio imefanya amekuwa kabisa. Hongera Mwana F.A.L.S.A.F.A

Umande
Автор

Leo naangalia ihi interview kwa Mara ya 25 na feel feeling ile ile since day one ilikua interview kubwa kwenye historia ya maisha yangu @salama wewe ni Bora zaidi kwenye izi Mambo

rahimuspinall
Автор

Huyu jamaa anajua na amezidi kunipa nguvu zaidi hadi sasa tunavyoongea nakuapia kwa mungu ntakuwa mfano mwema kama yeye ama zaidi yeye sababu ananikosha roho alafu maisha yake na yangu yameshahibiana amenitoa machozi

langemwepesi
Автор

Am a big fan of mwana fa since back then

ShawalAbdi
Автор

oohhh! leo ndio naisikiliza hii videos, now a day ndio mbunge MASHAALLAH

twahaally
Автор

Bigup to Salama, the interview is very inspirational. In our late 30+, I remember Mwanafa in his carrier and I can see what he has achieved in life. God bless.

abuuanwar
Автор

Nikiulizwa tofaut yako na watagazaji wengine (Hosts) nitasema wewe wewe sio host lakini unaweza kuwa zaidi yake. Kilichozidi kwako kuliko wengine ni uhalisia sana. Upo live sana wakat mwingine unaweza kumbadilisha mgeni wako katika mood tofaut tofaut na kupata ambacho watazamaji wako huwa tunayo shauku kwao

Mtu akitazama show yako kwa dakika 2 tu tayari anaingia live na anajihisi km sehemu ya mazungumzo yenu hata asitamani kuacha kutazama na kusikiliza show yako

Salama you're so live na Hongera

akiletv
Автор

Haya ni zaidi ya mazungumzo, yaani Salama ni mzuri sana ktk kuongea(anautajiri wa maneno)hali kadhalika Binadamu ndio kabisa.

mussamsella
Автор

So sad don't just judge pple and when you think you here seen a lot same pple walk in hell fire NEVER GIVE UP keep getting better MEHN I feel you FA thanks for the lesson

wedream
Автор

Duh imenigusa sana hii interview wallah cz yanafanana na maisha yangu japo yake yamezidi Mungu azidi kukupa ngivu ya kupambana na kuwapenda wanaokuzunguka 🙏

dicksonfondo
Автор

Aisee usione mtu anatembea au kula bhata... Achaaa tuu.. watu wanapitia magumuuuu sana. 🙌

rachelernest
Автор

Dah jamani acheni utani salama mzur nyie leo ndo nimeliona hili

rohityalsina
Автор

Salama akikuhoji inakufanya ufunguke zaidi, , anakufanya utoe exclusive, , wanaokubaliana namimi wapo ?

jamilaathumani
visit shbcf.ru