filmov
tv
Zee Maya - Kioo (feat. Josian) Official Video #emPawa100 Artist

Показать описание
Through the emPawa Africa initiative, Mr Eazi has selected 100 artists to receive $3000 each to create a music video.
Lyrics:
Yeah, Yeah, Zee maya
Sikujua, Yeah
Haikufaa iwe sasa, sijamaliza pingili za huu muwa
Na haitakaa iwe chafya ndio siri nitakayoamua
Kwani umezificha namba, nisipime kiasi
Kwa vile imekuja ghafla nashindwa nikubali basi
Nilichotamani usiishe tuendelee
Hatua ya kucheza mbali sikukubali initembelee
Niambie upepo au umeguswa
Nami sikumwaga nilipotoka,usisingizie utelezi umekuangusha
Kioo, haijatosha jiunge niziangalie chunusi
Kama nilikuwa nakosa usingerudisha matusi
Sawa mi nilikutumia, hata nje ya kazi zako
Nikamulika wapita njia, nicheke wakiumia macho
Basi ungetoa sauti nje na yangu unipinge
Sio ulivyokubali nyufa ili macho uyakinge
Nikitoka usiku nikakutupe, kesho nitaamka peke yangu
Na sitaki yanikute hautatangaza ya chumbani kwangu
Kioo, amekuvunja nani
mi nataka nitoke mbona nikitazama sionekani
Kioo, mi sio wa kwanza usinifunge
Niruhusu nikuite tena ukiniitika nikuchunge
Ulitembea nilipochoka
Kioo, kioo
Nakuhitaji haijatosha
Kioo, kioo usinipe
Sio kuniomba nguo tu, haukuwahi kuniomba nizime taa nisijione
Haukuwahi kuniomba niache niugue macho na nisipone
Haukuwahi kuvimba kukataa
kiasi cha kuficha umbo lako, nikiacha kusifia nitakubali sawa ulinifaa
Imeisha hali siwezi kuirudia
Taahira akiokota miba njiani nyayo timamu zinamsujudia
Sina we' tena mkononi
Na nakuomba nitakaposinzia unitembelee ndotoni
napojiandaa kuchekwa najua
Bila kiatu tope linauzaga soksi nipo njiani kununua
Nipo njiani kuinua macho ya wengi mtaani/ Nitakapokatiza huku nimeifunga tai begani
Unahisi mi sijajua, kwako nilikuwa tambazi
Wakati ili unilinde mi niliacha mlango wazi
Uliimba dansi nikakataa kucheza
Bado ukanipa kicheko hata nilichotoa baada ya kupoteza
Kioo,amekuvunja nani
mi' nataka nitoke mbona nikitazama sionekani
Kioo, isiwe mwisho nakuhitaji
Tangu umefahamu vya kwangu usiniache niitwe mkosaji
Ulitembea nilipochoka
Kioo, kioo
Nakuhitaji haijatosha
Kioo, kioo usinip
Sitakuuliza ulichobeba
Iwe kwa jua ama mawingu
Ukiinama nitakupa bega
Ibaki mchana au usiku
Niambie nitakuona tena
Au nitumie mfano wa maji kusahau, sema
Kioo, amekuvunja nani
mi nataka nitoke mbona nikitazama sionekani
Kioo, mi sio wa kwanza usinifunge
Niruhusu nikuite tena ukiniitika nikuchunge
Credits: Umaya Twaha, Jossian Wawency & Abdallah Abubakar
Keep up to date here:
#ZeeMaya #Kioo #Josian
Комментарии