Zee Maya - Kioo (feat. Josian) Official Video #emPawa100 Artist

preview_player
Показать описание

Through the emPawa Africa initiative, Mr Eazi has selected 100 artists to receive $3000 each to create a music video.

Lyrics:

Yeah, Yeah, Zee maya
Sikujua, Yeah

Haikufaa iwe sasa, sijamaliza pingili za huu muwa
Na haitakaa iwe chafya ndio siri nitakayoamua
Kwani umezificha namba, nisipime kiasi
Kwa vile imekuja ghafla nashindwa nikubali basi
Nilichotamani usiishe tuendelee
Hatua ya kucheza mbali sikukubali initembelee
Niambie upepo au umeguswa
Nami sikumwaga nilipotoka,usisingizie utelezi umekuangusha
Kioo, haijatosha jiunge niziangalie chunusi
Kama nilikuwa nakosa usingerudisha matusi
Sawa mi nilikutumia, hata nje ya kazi zako
Nikamulika wapita njia, nicheke wakiumia macho
Basi ungetoa sauti nje na yangu unipinge
Sio ulivyokubali nyufa ili macho uyakinge
Nikitoka usiku nikakutupe, kesho nitaamka peke yangu
Na sitaki yanikute hautatangaza ya chumbani kwangu
Kioo, amekuvunja nani
mi nataka nitoke mbona nikitazama sionekani
Kioo, mi sio wa kwanza usinifunge
Niruhusu nikuite tena ukiniitika nikuchunge

Ulitembea nilipochoka
Kioo, kioo
Nakuhitaji haijatosha
Kioo, kioo usinipe

Sio kuniomba nguo tu, haukuwahi kuniomba nizime taa nisijione
Haukuwahi kuniomba niache niugue macho na nisipone
Haukuwahi kuvimba kukataa
kiasi cha kuficha umbo lako, nikiacha kusifia nitakubali sawa ulinifaa
Imeisha hali siwezi kuirudia
Taahira akiokota miba njiani nyayo timamu zinamsujudia
Sina we' tena mkononi
Na nakuomba nitakaposinzia unitembelee ndotoni
napojiandaa kuchekwa najua
Bila kiatu tope linauzaga soksi nipo njiani kununua
Nipo njiani kuinua macho ya wengi mtaani/ Nitakapokatiza huku nimeifunga tai begani
Unahisi mi sijajua, kwako nilikuwa tambazi
Wakati ili unilinde mi niliacha mlango wazi
Uliimba dansi nikakataa kucheza
Bado ukanipa kicheko hata nilichotoa baada ya kupoteza
Kioo,amekuvunja nani
mi' nataka nitoke mbona nikitazama sionekani
Kioo, isiwe mwisho nakuhitaji
Tangu umefahamu vya kwangu usiniache niitwe mkosaji

Ulitembea nilipochoka
Kioo, kioo
Nakuhitaji haijatosha
Kioo, kioo usinip

Sitakuuliza ulichobeba
Iwe kwa jua ama mawingu
Ukiinama nitakupa bega
Ibaki mchana au usiku
Niambie nitakuona tena
Au nitumie mfano wa maji kusahau, sema

Kioo, amekuvunja nani
mi nataka nitoke mbona nikitazama sionekani
Kioo, mi sio wa kwanza usinifunge
Niruhusu nikuite tena ukiniitika nikuchunge

Credits: Umaya Twaha, Jossian Wawency & Abdallah Abubakar

Keep up to date here:

#ZeeMaya #Kioo #Josian
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Kichupa kikali balaa! Iko perfect sana hii ngoma. Big up sana Zee Maya

jumaibrahim
Автор

Very creative, very unique lyrics, napenda mziki mzuri, this is good music, keep this good work up bro. Bless.

MegaPhage
Автор

Kama una mkubari zee Maya gonga like hapaa

homan_nkwama
Автор

Maya respect kwako bro kaza buti mungu ni mwema kama wengine wametoka hata ww pia utatoka Maya, nakuombea kwa mungu sana

musamwaweza
Автор

Haichoshi kuisikiliza na kuangalia ninj real hip hop keep it boy

kapayabunzali
Автор

ngoma Kali nimeirudia zaid ya Mara kumi, namuona mwanafalsafa part 2

maxnzarombi
Автор

Haya ndio mapinduzi tunayo taka big up sanaaah

homan_nkwama
Автор

itz perfect zee maya gat u ma blood one

lusajoraphael
Автор

Love from LOS ANGELES
GRACIAS 👽🖖💛💛💛💛💛

AngelicaPelayo
Автор

nimeichek dg ang iko kali hicho kuchupa, rangi nzuri tartbu tutafika

peternchimbi
Автор

Jossian do great things in this featuring

BobsamEugen
Автор

MUCH LOVE BROTHER YOUR MUSIC IS SO REAL .MUCH LOVE TOKA +254

tjbwoy
Автор

#ZEE_MAYA KAKA HONGERA KWA UWEZO WA UTUNZI

herryshabanimakomberasimba
Автор

Hongera bro
Video kali sana
Endelea kukaza one day yes

benedictomihayo
Автор

jamn maya hata siamin daaaa umenikosha jamn aiseeee songa mbele kaka nipo nyuma yako nataman nifike hapo

neemajohn
visit shbcf.ru