MADAKTARI HOSPITALI YA SELIANI ARUSHA WAGOMA WAGONJWA 'WAHAHA'

preview_player
Показать описание
#wepesimedia #wepesitv

Watumishi zaidi ya mia mbili wanaotoa huduma za afya katika hosptali ya Selian Jijini Arusha, wamegoma kufanya kazi ya kutoa huduma kwa zaidi ya saa tano kwa shinikizo la kutaka kuonana na uongozi wa hosptali hiyo kutokana na madai yao ya mishahara ya miezi sita.

Miongoni mwa watumishi waliozungumza na waandishi wa habari hosptalini hapo wakiomba sura zao zisionekane wala kutajwa majina yao, wamesema asubuhi ya Julai 01, 2024 saa mbili asubuhi wote kwa pamoja waliomba kuonana na Uongozi wa Hosptali hiyo ili kuzungumzia changamoto ya mishahara, lakini Uongozi huo ulikaidi ndipo waliamua kusitisha kutoa huduma kwa wagonjwa.

Aidha, wamesema baada ya kusitisha huduma kwa zaidi ya saa tano, Uongozi wa Hosptali hiyo uliwaita na kuzungumza nao kwa ombi kuwa warejee kufanya kazi na itakapofika Julai 04, 2024 suala hilo litakuwa limeshughulikiwa, huku ikidaiwa kuwa kauli ya matuini ya kulipwa mishahara yao imekuwa ikitolewa mara kwa mara bila utekelezaji wowote.

CC 🎥 @gaditvonline
Рекомендации по теме
join shbcf.ru