Harambee Stars imeishinda Chipolopolo ya Zambia 2-1

preview_player
Показать описание
Kikosi cha taifa cha Harambee Stars kilipata ushindi wa mabao 2 – 1 dhidi ya Zambia katika mechi ya kirafiki iliyoandaliwa ugani Nyayo bila mashabiki.
Wenyeji walijipata kifua mbele kupitia bao la kujifunga baada ya mchezaji Tandi Mwape kufanya masihara katika eneo la hatari. Mchezaji Cliff Nyakeya aliifungia Harambee Stars bao la pili muda mfupi baadaye na kuipa Kenya uongozi wa mabao mawili kufikia muda wa mapumziko. Katika kipindi cha pili, mchezaji Emmanuel Chabula aliifungia Chipolopolo bao la kufuta machozi. Harambe stars sasa itakwaruzana na timu ya taifa ya Comoros novemba tisa katika uga wa Nyayo.
Рекомендации по теме
welcome to shbcf.ru