UJENZI WA MWENDOKASI MBAGALA, GONGOLAMBOTO KUANZA DESEMBA, 2018

preview_player
Показать описание
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais ametangaza kuanza kwa ujenzi awamu ya pili na tatu ya mradi wa DART unaotarajiwa kuwa Decemba mwaka huu, ambapo jumla ya Dola za Marekani 289.91 Milioni zinatarajiwa kutumika kwa mkopo kutoka Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika.
awamu ya pili ya ujenzi wa miundombinu ya DART utakaohusisha barabara za Kilwa, Kawawa, Sokoine, Gerezani, Bandari na Chang’ombe zenye urefu wa Km 20.3 utakaogharimu Dola za Marekani Milioni 141.71.
awamu ya tatu ya ujenzi wa miundombinu ya DART utakaohusisha barabara za Nyerere, Uhuru, Bibi Titi, Azikiwe, Shaurimoyo, Lindi na Maktaba zenye urefu wa Km 23.6 utakaogharimu Dola za Marekani Milioni 148.2.
Рекомендации по теме