ANGALIZO LA TCU KWA WAOMBAJI WA VYUO 'HAKUNA KUBAHATISHA'

preview_player
Показать описание
Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Profesa Charles Kihampa amezungumzia wahitimu wanaohitaji maombi ya Vyuo vya Elimu ya Juu kuzingatia umakini katika uombaji kwa sababu hakuna kubahatisha.

Prof.Kihampa amesema wanaoomba maombi hayo wanapaswa kuomba kupitia tovuti za vyuo husika na yatafanyika kwa njia ya Elektroniki.

"Wanatakiwa kusoma miongozo inayotakiwa, hivyo waombaji wasome kwa umakini kwani hapa hakuna kubahatisha na asijaribu kuomba kwani hawatopata, hivyo waombaji waingie katika vyuo husika,"
Рекомендации по теме