Mafunzo ya Kuwasaidia Watoto Kupumua yamalizika Mwanza

preview_player
Показать описание
Inaelezwa kwamba takribani asilimia 10 ya watoto wanaozaliwa hukumbana na matatizo ya kupumua vyema na hivyo kuhitaji usaidizi wa kupumua kutoka kwa wahudumu wa afya ili kuokoa maisha yao.

Ni kutokana na umuhimu huo, Chama cha Watoa Huduma za Afya Tanzania APHFTA kwa kushirikiana na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho kutoka Marekani, kimeamua kutoa mafunzo kwa watoa huduma za afya kutoka Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali binafsi Kanda ya Ziwa ili kuwajengea uwezo wa kuwasaidia watoto kupumua wakati wa kuzaliwa, ambapo mafunzo hayo yamedumu kwa siku tatu Jijini Mwanza.
Рекомендации по теме
join shbcf.ru