OKA waahirisha tena hafla ya kusaini mkataba wa makubaliano

preview_player
Показать описание
Kwa mara ya pili muungano wa One Kenya Alliance-OKA umeahirisha shughuli ya utiaji sahihi mkataba wa makubaliano kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti. Viongozi wa muungano huo wanasema wanahitaji muda zaidi kujadili yale waliyotaja kuwa masuala ibuka ya kisheria kuhusiana na mkataba huo. Kiongozi wa chama cha NARC-Kenya Martha Karua alisema muungano huo bado umejitolea kudumisha umoja na utatangaza baadaye siku ambayo utatia sahihi makubaliano hayo.

Connect with KBC Online;

#KBCchannel1 #politics #OKA
Рекомендации по теме