Athanas Yakobo -NI BWANA (Official Music Video)

preview_player
Показать описание
Yohana 21:7
[7]Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, Ndiye Bwana. Naye Simoni Petro, aliposikia ya kwamba ni Bwana, akajifunga vazi lake, (maana alikuwa uchi), akajitupa baharini.
...............
kuna Mambo yanatokea au kupitia kwenye Maisha yetu lakini tusijue kuwa ni NI BWANA Katenda, hapo Petro hakujua. Mwanafunzi Ambaye Yesu alimpenda alijua kuwa NI BWANA, na Kwa Sasa huyo mwanafunzi ni wewe. Hivyo, yakupasa ujue kuwa Bwana ana uwezo wa kutenda makuu Juu ya watu wake na Uwaambie wengine walio uchi (kama alivyokuwa Petro), wenye uchungu mwingi, waliokata tamaa, wanaoteswa na masumbufu ya Dunia kuwa NI BWANA awezaye kufanya ukurasa mpya.

Mungu wetu siyo mnyonge, ni Mungu Mkuu Mwenye kujibu Kwa Moto (1Falme 18:24, 38-39), Mwenye kujidhihirisha Kwa tanuru ya Moto, umeme/radi, Ngurumo, Moshi na Mwenye kutetemesha milima, Mwenye Neno linalopasua mawe, Mwenye kuipasua bahari n.k (kutoka 19:16-18, Mwanzo 15:17, Yeremiah 23:29). Lakini kama apendavyo yeye anaweza akajitwalia umbo la upole, na unyenyekevu mwingi na akaja kwako Kwa sauti ya upole na utulivu (Mathayo 11:29, 1Wafalme 19:12).

Katika namna zote tujue kuwa NI BWANA.

Namshukuru Sana Mungu Roho Mtakatifu aliyenipa Melody ya wimbo huo mnamo tar 29/01/2023 usiku ndotoni. kama kutukuzwa atukuzwe yeye.

Zaburi 115:1
[1]Ee BWANA, kutukuza usitutukuze sisi,
Bali ulitukuze jina lako,
Kwa ajili ya fadhili zako,
Kwa ajili ya uaminifu wako.

Singer and song writer: Athanas Yakobo

Song: NI BWANA

Audio Producer : Eng. Golden fingers

video producer: Director Meek

MAY GOD BLESS YOU !
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Oooh Alleluia hakika ni Bwana Mimi nimeshuhudia kwa macho yangu kwamba ni Bwana.haki uuuh wimbo umejua kunibariki

dianamutahaba
Автор

Sanduku la Agano limeturejea, Ni Bwana hakuna mfano wake.

prosperogola
Автор

Mkono wa Bwana umetuinua. Ni Bwana❤ hakuna mfano wake. Hongera sana Mtumishi Athanas Yakobo

prosperogola
Автор

Ni Bwana amejibu maombi

Hajaacha mtesi ajitutumue...💥💥💥💥💥

DonaJr
Автор

Amejibu kwa kushindo!!!!Hongera sana Mtumishi wimbo mzuri mno!!!!

christinamwingira
Автор

Hallelujah, Ni bwana akuna mfano wake, barikiwa sana Mtumishi

josephhuberty
Автор

Hongera Sana Mungu azidi kupandisha viwango vya juu sana

samweljulian
Автор

Kazi nzuri kaka, , kadiri siku zinavyokwenda ubora wa Kazi unaimarika na unakwenda vile muziki unataka

hamisimussa
Автор

Mkono wa Bwana uendelee kuwa juu yako Mtumishi wa Mungu, nimebarikiwa kwa wimbo huu❤

jamesmayunga
Автор

Hongera sana Brother...God is always able, another blessing...wimbo mzuri..🙏

nicetasangelo
Автор

Ooh waooh keep it up nimebarikiwa saana

JudithEvarister-vo
Автор

hongera brother kazi nzuri . #Eng INNO G&B

official_c
Автор

Hongera sana Atanasi. Aluta continuer no turning back

doreenarbogast
Автор

Nimebarikiwa sana. The song is as humble as the singer.

amanijm
Автор

Nice Yakobo!. This is the only way up best one that every one of us admires and u see u take a gut to present us all!. Keep Moving chief seeing u far far far above the sky thats what God tells over the future🙏!

josephjosephat
welcome to shbcf.ru