JIRANI ALIYEFIKA MOCHWARI KUSHUHUDIA MKE na MUME WALIOKANYAGWA na BASI, ASIMULIA ALICHOKIONA..

preview_player
Показать описание
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera linamshikia dereva wa basi la Happy Nation, Shabani Khatibu (38), mkazi wa Dar es Salaam kwa kosa la kusababisha vifo vya watu 2; mume na mke ambao ni Geofrey John (42) ambaye ni mfanyabiashara na Tumaini John (41) ambaye ni Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Maruku, wote wakazi wa custom Manispaa ya Bukoba baada ya basi hilo kugongna na pikipiki.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, ACP William Mwampaghale amesema ajali hiyo ilitokea Desemba 6, 2022 muda wa saa tano na nusu asubuhi katika Barabara ya Biharamulo Kata ya Ijuganyondo katika Mansipaa ya Bukoba ambapo gari lenye namba za usajili T-705 DFV aina ya YOU TONG, mali ya Kampuni ya Happy Nation, likitokea Dar es Salaam kwenda Bukoba liligongana na pikipiki yenye namba za usajili T-308 CLH aina ya SANLG iliyokuwa inaendeshwa na Geofrey John na kusababisha kifo chake papo hapo pamoja na abiria aliyekuwa amempakia ambaye ni mkewe Tumaini John.

⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:

⚫️ JE, NA WEWE UNA HABARI?
⚫️ WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE: ( +255 657 693 210), ( +255 713 750910)

⚫️ OUR PLAYLISTS:
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Mtihani poleni wafiwa mungu awatiye nguvu

sabihahamadi
Автор

Poleni sana anko kwa kuondokewa na majirani zako.

felixbenos