HOTUBA KAMILI YA RAIS MAGUFULI AKIWA TARIME - 07/09/2018

preview_player
Показать описание
Ni kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo Septemba 7, 2018 kwenye Chuo cha Ualimu Tarime ikiwa ni sehemu ya ziara yake mkoani Mara.

Katika kuhitimisha ziara yake mkoa wa Mara, Rais Magufuli amehutubia mkutano wa hadhara Mjini Tarime na kuwahakikishia wananchi wa mji huo kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kuwahudumia wananchi bila kuwabagua.

Katika hotuba hii Rais Maguli ameeleza sababu ya kumuondoa kwenye nafasi yake Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Valentino Mlowola, amekemea vitendo vya rushwa na ubadhirifu ndani ya CCM, pia amemkaribisha CCM mbunge wa CHADEMA Ester Matiko.

Amesema kwamba kwa Tarime serikali imetenga shilingi Bilioni 14 kwa ajili ya mradi mkubwa wa maji, imeanza ujenzi wa barabara ya Tarime – Mugumu kwa kiwango cha lami, imetoa shilingi milioni 400 za ujenzi wa kituo cha afya, inatoa fedha za elimu bila malipo kila mwezi na inaendelea kusambaza umeme kwa vijiji vyote visivyo na umeme.

Rais Magufuli amezungumzia uwekezaji wa shamba la miwa na kiwanda cha sukari katika wilaya ya Tarime, na kueleza kuwa Serikali itafanya uchambuzi wa kina kabla ya kuridhia mradi huo huku akiwataka viongozi wa Mkoa na Wilaya kuondoa tofauti zao.

Kwa wilaya jirani ya Rorya Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo kutafuta fedha kiasi cha shilingi Bilioni 1.5 kwa ajili ya kujenga hospitali.
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Loooo! Ni hasara na pengo sana kumpoteza kiongozi wetu mkubwa kama huyu. Maskini watanzania. Tutampata wapi tena. Mungu twakuomba iweke roho ya baba yetu Rais wa Tanzania. J.M. Amina.

stellakutta
Автор

Mwenyezi mungu akupumuzishe mahali pema peponi amen

josephgervas
Автор

Mungu akukumbuke akumbuke sadaka yako uliotoa wakati wa uhai wako.akusamehe makosa yako.akupe Raha ya Milele.

machoguhameri
Автор

Tulikupenda sana mh JPM mungu akulaze pema

christiankambuga
Автор

Yaani ni hasara. Tulipoteza kiongozi wa ajabu sana. Alikuwa ni kiongozi mwenye hekima, busara, maarifa, akili zuri za kuwaongoza Watanzania. Loooo! Ni pengo sana lisilozibika. Mungu iweke roho ya Tas wetu Marehemi

stellakutta
Автор

Yumekumis sana baba jpm pumzika kwa amani mwanga wa milele ukuangazie

husseinhamiss
Автор

Mungu akutangulie, kweli wewe ni chuma.tangulia BABA.Mungu atakulipia.

karimhgau
Автор

Duu! Alaaniwe kama kuna alie husika na kifo chako rais wetu. Nakuelewa sana

edwardmagige
Автор

naendelea kumwombea huyo Rais JPM Usiku na mchana, Mungu amjalie katika uongozi wake! Anafaa kuitwa Rais wa Afrika nzima!

nendemakyambe
Автор

😭🇹🇿😭🇹🇿😭🇹🇿😭🇹🇿😭🇹🇿😭Hakika hayati Dr John pombe Magufuli Tutamkumbuka daima kipenzi chetu

samwelilaizer
Автор

😭😭😭😭😭😭😭tutayaishi mema yako huruma zako na upendo wako kitabu chako nikizurii sana pumzika baba tunakuombea

amourmunga
Автор

vizuri saana Rais Magufuli kwa hotuba nzuri

wamburachacha
Автор

Keep shinning wherever you are! Missing you Big Man ..

ndimamsuya
Автор

Aisee m/mungu akusamehe makosayako uliweza kwa kiasichako sizani kama tutapata atakae kulivu

jumakalukule
Автор

Nita kuku mbhuka sana rais wangu mwenye upendo wadhati uliyo tuonesha sisi watanzania tunakujua vizuri sana mungu akutangulie uko uliko tuta endelea kuku penda auta futika katka moyoni mwetu utabaki daima rais wangu mwenye upendo wadhati na bara la Africa mwenyezi Mungu na ombha utulinde na kila shari

karimhgau
Автор

Upumuzike kwa Amani na Mwanga wa milele ukwangazie ehee bwana!Apumzike kwa Amani...Amina

raphaelkailembo
Автор

Daah Rest in peace My President John, now mzee Tz ni nchi ya tozo, na kusifiana tuu pasi utelekezaji, wale wote uliowateua washapigwa chini, nchi ishabiki chungu #Samia mwenyewe kila day Safari zisizoeleweka My President Rest in peace Baba Magufuli🕊

smootkizy_jr
Автор

The only hero of our time....baada ya mwalimu nyerere kiongozi pekee anayefuata ni huyu...hakuna mwingine. Mpaka leo Mungu ametupa viongozi hawa tu

richardboaz-mashagospel
Автор

I never get enough of him. He went too soon🙏

alcoholdisque
Автор

Muheshimiwa alivyosema "Pendaneni, Shirikianeni Msibaguane" jozi limetaka kunitoka". Kila Muheshimiwa Rais akimtaja mkuu wa wilaya msaidizi wa Rais anamwangalia kwa jicho kali mkuu wa wilaya 💪👊, ila anaonekana mtu wa huruma kwa sababu ana tabasamu mara kwa mara.

salehsports