Rais mteule Trump akutana na Rais Biden

preview_player
Показать описание
Rais-mteule wa Marekani, Donald Trump Jumatano alikwenda White House kwa mara ya kwanza baada ya miaka minne kukutana na Rais anayendoka mamlakani Joe Biden.

Biden alimkaribisha Trump kwa ziara ya kawaida, kuonyesha kuwa Januari 20 kutakutwa na makabidhiano ya amani ya madaraka katika demokrasia ya Marekani kati ya kiongozi wa sasa wa Marekani na mtendaji mkuu anayeingia katika wadhifa huo. Utamaduni wa wa kumkaribisha rais anayeingia madaraka ni moja ya jambo ambalo Trump hakulifanya baada ya Biden kumshinda mwaka 2020. Mkutano wa Jumatano kati ya watu hao wawili ulikuja wakati Trump akichukua kuunda utawala wake.

“Ndiyo, Bwana Rais-mteule na rais wa zamani Donald Trump, hongera sana na natazamia kRama nilivyosema, kuw na makabidhiano ya amani ya utawala. Tutafanya kila kituo tunachoweza kukidhi kile unachokihitaji na ndiyo tutapata fursa ya kuzungumza kuhusu baadhi ya mambo hayo hivi leo. Karibu, karibu tena.”

“Ahsante sana. Siasa ni ngumu. Na katika nyakati nyingi, si sehemu nzuri sana katika dunia. Lakini ni dunia nzuri ya leo na nashukuru sana. Kipindi cha mpito kitakuwa hakina tatizo mambo yatakwenda vizuri na nashukuru sana kwa hilo, Joe,” amesema Rais-mteule Trump.

Mke wa Rais Jill Biden alijiunga na mume wake kumklaki rais-mteule alipowasili White House. White House imesema alimpa Trump barua ya pongezi aliyomuandikia mke wake, Melania, na kuelezea kuwa timu yake iko tayari kusaidia katika kipindi cha mpito.


#rais #donaldtrump #kamalaharris #wafuasi⁣⁣⁣
#voaelections ⁣⁣⁣⁣⁣⁣⁣⁣
#voaelections2024
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Ngozi nyeupe inaneema Africa ata kiongoz wa familia tu ni vigisu na wivu mungu anapnda hv upendo na aman

Mihoaidan
Автор

Rais wa Marekani wanajua kuwa Ikulu sio Mali yao Ikulu ni wananchi wa Marekani!!

simonnaivasha
Автор

Kutafsiri live conversations ni uchaguzi wa maana nzima ya tukio. Take it frome

kaisarimbisso
Автор

Hivi kweli hii inaweza kutokea kwenye nchi zetu kama Tanzania?

WILSONMBWAMBO-szzu
Автор

Mcha Mungu kakutana na liabudu shetani

gilbertkalanda
join shbcf.ru