Ambwene Mwasongwe - Unikumbuke (Official Music Video)

preview_player
Показать описание
Ambwene Mwasongwe presents the Official Music for "Unikumbuke"

Follow Ambwene Mwasongwe

Digital Branding & Marketing By:

Ambwene Mwasongwe - Unikumbuke

Nimekuita uambie watu ushuhuda wangu
Miaka tisa nimekaa jela
Nilifungwa kwa kosa la kusingiziwa
Namshukuru Mungu nimetoka

Usiku ule nilikamatwa kama mchezo
Na mke wangu na mtoto mdogo
Nikadhani labda walikuwa wanatania
Labda ilikuwa siku ya wajinga

Hakuna mtu alielewa ukweli wa ushahidi wangu
Wala sikuwa na wakumweleza akanielewa
Mazingira ya kesi, ushahidi, sheria za kazi
Siri ni ban, mpaka mke wangu kaniambia
Kama umefanya kiri kosa tujue moja

Nikumbuke, kumbuka haki yangu, sikufanya ubaya
Nikumbuke, nikumbuke, sikufanya ubaya
Nikumbuke, namna walivyonishtaki kwa hila na wivu
Nikumbuke, bwana unikumbuke nililia
Hey, kumbuka bwana haki yangu

Hey, wakumbuke, walivyo kufanikiwa jela
Uwakumbuke, Mungu wakumbuke washa mshumaa ndani ya nyumba
Mkumbuke mtoto mchanga asiye na hatia
Uwakumbuke, kama ningekuwepo angekonda
Kumbuka Adam, aliyebaki, alikufanya kushtuka kwa ajili yako
Nilidhani Mungu kalisahau faili langu

Nikadhani kwamba nitaaibika
Sikuwa tena na tumaini lililobaki
Haki yangu ilikuwa tumaini pekee
Waweza elewa shahidi wangu alikuwa Mungu
Labda na wale walioua
Mwisho wa siku Mungu alinitetea

Na waliofanya kosa kunikana
Haki yangu ikasitana kama mtende na mwelezi
Pale banoni, walinichimba wakuning'oa sababu ya Mungu
Waliinamisha wakunivunja, walinitikisa sikupukutika
Walinichuma ili niishe

Wewe bwana ulinitetea na haki yangu
Nikumbuke, kumbuka maadui walivyonizunguka
Nikumbuke, kumbuka ushahidi wa maneno yao
Nikumbuke, kumbuka walivyonichafua jina langu
Nikumbuke, kumbuka walivyoniona

Mi ni mhalifu, hey ukalisafishe jina langu
Hey bwana, uwakumbuke! Uwakumbuke Ukarehemu makosa yao
Uwakumbuke! Japo walifanya ubaya bwana na uwasamehe
Uwakumbuke! Nilienda jela nikiwa bado sikujui
Uwakumbuke! Nimetoka nimeokoka nimekujua
Nikumbuke! Bwana unikumbuke usinisahau
Natengeza fadhili zako, niimbe Mungu baba

Nimefurahi, niimbe Mungu bwana
Nimefurahi, niimbe Mungu bwana
Nimefurahi, niimbe Mungu bwana
Nimefurahi, niimbe Mungu bwana

#AmbweneMwasongwe #Unikumbuke
Рекомендации по теме
Комментарии
Автор

Nilifatilia history yauyo jamaa mwanajsh aliefungwa bilakosa nakupoteza mke namtt Mungu ambariki bado anampend

starlonejadamskp
Автор

Nmemwona huyo mwanajeshi aliyefungwaga bila hatia i hope uliimba kwa ajili yake, kama umemnotice huyo mjeda...nipe likes

carlosleonard
Автор

😭😭😭 Kuna watu wanapitia pagumu!! Mungu kutana na watu ambao wanapitia pagumu na wanasikiliza huu wimbo, wakumbuke Bwana!!!

beatriceminja
Автор

Mungu nikumbuke nimefiwa wazazi wote ndoa nayo nanyanyasika kupigwa kila mwezi, ndugu zangu hawaamini wanasena nataka kwenda kufanya umalaya, nikumbuke mungu 😭😭😭

magenisweke
Автор

Kama uliwahi kupita mapito magumu na kudhani kabisa hutoweza kuvuka😭😭😭mara pap! Ukayavuka lazima ukisikia huu wimbo ulie😭😭😭 ASANTE BWANA KWA KUNIKUMBUKA 😭😭😭

deodatusmwacha
Автор

MUNGU naomba unikumbuke na mimi 🤲🤲🤲🧎‍♀️🧎‍♀️🧎‍♀️😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭, , , naomba sana MUNGU

TelesinaSinai
Автор

Eee Mungu uikumbuke Tanzania yetu Mauwaji yamekua mengi sana 😭😭😭😭 tusamehe uturehemu na ututakase Yesu 🙏🏼🙏🏼 turudishie kupendana na kuchukuliana madhaifu tunaomba Baba 😭😭🤲🏾. Amen

kettyym
Автор

Kupitia wimbo huu MUNGU akawafariji n kuwakumbuka wote wanaopitia magumu
amiina

NadhifaDauda
Автор

Hakika sio wote wanaokwenda jela wamekosa, wengine wanasingiziwa tu.
Wimbo huu unanikumbusha nina rafiki yangu tuliyesoma wote kozi ya utabibu CO mwaka wa kwanza then akahamia chuo kingine baada ya kumaliza mwaka wa pili akabambikiziwa kesi ya kumbaka hadi kufa mtoto wa kaka yake akaenda jela ila baada ya mwaka mmoja ikabainika amesingiziwa daaah so pain, Mungu ndio mtoa haki ahsante sana kaka ambwene napenda sana tungo zako ujumbe katika nyimbo zako.

kelvinlukoo
Автор

Ee mwenyezi Mungu mkumbuke uncle wangu najua hana hatia 😭

racheljob
Автор

Ambwene ni mwimbaji wangu bora kabisa wa gospel tangu ule wimbo misuli ya Imani hajawahi utukumbuke eeh Yesu Kristo wa Nazareth 😭🙏🏻

georgenathanael
Автор

nimemuona huyu jamaa aliyesingiziwa kesi hiyo kweli kweli Mungu huwa anasababu ya kila jambo haijawahi kuwa rahisi kaka samehe kunajambo Mungu ameakuandalia sehemu mwanandamu hakupanga au kupaswa kujua haikuwa bureee, nahisi huzuni sio huruma na ninaamini katika Kristo anayeishi Utakuwa mkuu siku moja, Amen

extremedrivingTanzania
Автор

Sio wote walioko jela n wakosaji ama Wana hatia ila n kwamba tu wamejikuta either kusingiziw ama jumba bovu kuwaangukia ee mungu usikiaye maombi Kila aliejikuta uko bila hatia jua la haki likamzukie na ukamkumbuke...hakika Ambwene mm huwa najikuta nasikilz nyimbo zake natokwa tu na machozi ....

emanuelmbise
Автор

Wimbo huu unaniumiza sana kila nkikumbuka hii story ya mauaji mwaka 2006 ubungo mataa (Kijazi Interchange), huyo main character kwenye video ndio alikutana na huu mkasa kukaa miaka tisa kwa kesi ya kusingiziwa an. Ila Mungu mkubwa na anataendelea kumuweka juu ya maadui zake. Amen

stivertz
Автор

MUNGU akufunge mkanda kaka Nazareth kaka ambwene ubarikiwe kwakufariji wengi tuliovunjika moyo

sevelinamwailanga
Автор

Hakika wimbo ni mkubwa sana huu watanzania, Mungu amtunze hakika

cosmasarnold
Автор

Mm uwa nalalamikasana kumbe wapowatu wanapitia magumu zaidi yangu mungu nisamee kwaku laumu kwangu leo nimeji fuza kitu kupitia uwimbo iposiku namm tabasamu langu nitalejea tena mungu nimwaminifu sanaa 🙏🙏🙏

Alviq-ip
Автор

Mwezi mungu nikumbuke baba nime pambana sana jmn lkn sioni tumaini langu

ErickKimaro-bfzs
Автор

Unaweza guswa na Habari ya Yusuphu, kumbe hata sasa Kina Yusuph wengine wangali wakionesha ukuu wa Mungu, Akhsante Mungu kuyashuhudia haya katika macho yangu, Wewe ni Mungu wa Nyakati Zote, Ambwene Ambwene

jeremiahmsangi
Автор

Nimeisikiliza story ya Kaka Nazareth kwa Milard Ayo! Atukuzwe Mungu sana kwa kumuinua na kumuokoa mtumishi wake

rehemaeli
welcome to shbcf.ru