TAIRI YAPASUKA NDEGE IKIWA INAKARIBIA KURUKA

preview_player
Показать описание
Video ikionyesha tairi la ndege ya Shirika la Ndege la Marekani lilipolipuka wakati ndege hiyo ikijiandaa kuruka kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Tampa.

Rubani alisitisha kuirusha ndege hiyo, na kuiegesha pembeni ambapo baada ya muda mfupi magari ya dharura yalifika kutoa msaada zaidi.

Msemaji wa uwanja huo wa ndege, Joshua Gillin, ameviambia vyombo vya habari vya eneo hilo kuwa abiria wote 174 pamoja na wafanyakazi sita waliokuwa ndani ya ndege hiyo walitoka salama na kwamba abiria wote walipatiwa ndege mbadala kwenda Phoenix.

Je una habari ama tukio lolote? Tupigie kupitia #0768811595
Instagram: @tanzaniaweb
Facebook: @tanzaniaweb
Twitter: @TheTanzaniaWeb
visit shbcf.ru